Sifa za Mwanaume wa Ukweli Chini ya Jua !

SIFA YA MWANAUME WA UKWELI, SI KUWA NA VIBINTI, VIBICHI VIBICHI, BALI TUTAKUPIMA KATIKA MAMBO YAFUATAYO ! Ujanja wa mwanaume si kujua kutongoza wasichana. Imekuwa kama kadesturi miongoni mwa vijana tuliowengi ,tulioibukia katika kizazi hiki kinachoifahamu computer kuliko kitu kingine. Kizazi kichoifahamu Google kuliko mlango wa kanisa au msikiti inashangaza.Mithili ya watu tuamkao toka usingizini tumepigwa na butwaa na bumbuazi limetuenea mawazoni hatuna cha kusema mbele ya dunia ya mavumbuzi. Tumeshindwa kujiongoza,tumeyakubali matakwa ya mwili pamoja na tamaa iongoze mstakabari wa maisha yetu. Tumeona ni ni ujanja na ufahari kuwa na mademu wengi,kuliko kuhangaikia mambo ya msingi kwa ajili ya kesho inayo kuja mithili ya upepo wa kimbunga. Tumekuwa washamba wa mapenzi na ulimbukeni usio na sababu ndio unao tuliza kila iitwapo Leo kwa sababu tumeingia kichwa kichwa katika mapenzi tukidhani ni kama kunywa chai, kumbe tumejipeleka vitanzini kwa hiari. Amakweli si kila anayejiita”born...